Wewe shetani muongo.....nipishe njia, wawadanganya watu wa Mungu, ondoka njiani kabisa!!!! niende kwa Bwana Yesu......nipishe niende nipate neema zake. Yesu wangu ameniita....nipishe mimi niende, kutangaza habari njema. Sio mtumwa wako tena, tangu leo mimi ninakukana kabisa!
Umewadanganya wengi kwa ahadi za uongo, wanauwa ndugu zao wapate kutajilika....ondoka njiani kabisa shetani mbaya wee.....nipishe mimi niende, kwa Yesu Mkombozi wangu, ubaki na uongo wako. Yesu wangu ameniita, kutangaza habari njema kwa watu wote, tangu leo ninakukana kabisa sio wangu tena shetani mkubwa we!
Umewadanganya watu wengi kwaajili ya anasa, wametoa mimba zao....hawataki kulea watoto wao. Umewadanganya wengi wamekimbia miji yao, wameacha familia kwaajili ya nyumba ndogo....ondoka kabisa hapo njiani, nipishe mimi niende kwa Yesu Mkombozi wangu mwema, ubaki na uongo wako. Umewadanganya mabinti wengi wanauza miili yao, wanaitwa machangudoa, eti hiyo kwao ni ajila.....ona aibu wewe shetani!
No comments:
Post a Comment