Tuesday, November 29, 2011

NYANYA ZA KIPERA - MLALI - MOROGORO - TANZANIA.

Zao la nyanya ndio zao kuu la biashara kwa wakazi wa Kijiji cha Kipera na vitongoji vyake. Wakazi wengi wa Kijiji hicho kilichopo Kata na Tarafa ya Mlali, Wilayani Mvomero, Mkoani Morogoro...hulima nyanya kwa wingi msimu wa kilimo unapowadia na wafanyabiashara hufika Kijijini hapo na kununua zao hilo na kusafirisha hadi Jijini Dar es salaam au Mikoa mingine Tanzania.

Pichani ni moja ya Kijana mkazi wa Kijiji cha Kipera, ambaye mbali na kulima zao hili anasema; ''msimu ukifika ni ajira kwa kila mtu Kijijini hapo alimaye na asiyelima nyanya. Anasimulia kuwa wapo ambao hujishughulisha na uvunaji wa nyanya mashambani, usombaji kutoka shambani hadi vilinge vya wafanyabiashara, upangaji katika matenga...kama afanyavyo yeye na upakiaji katika magari.'' Pia anasema wapo wanaofanya kazi ya kukata majani kwaajili ya kupangia nyanya hizo katika matenga. Anasema; msimu wa mavuno ya nyanya wafanyabiashara wengi sana hufika Kijijini hapo hivyo akina mama na watu mbalimbali hufungua migahawa ya chakula na kufanya pato la wakazi wa Kijiji hicho kukua kipindi hicho. Lakini analia na bei ambayo mkulima hupata, ambapo tenga moja la kuingia plastiki 3 za lita 20 hununuliwa kwa kati ya Tsh.5000 na 8000/= kulingana na ubora wa nyanya ulizonazo. Ipo haja ya Serikali kuharakisha ukamilishaji wa ujenzi wa Kiwanda cha kusindika nyanya Kijijini hapo ili kukuza kipato cha wakazi wa Kijiji cha Kipera.




Nyanya hii ikifika Jijini Dar es salaam, huuzwa kwa bei ya juu sana!




No comments:

WATEMBELEAJI