Tuesday, March 27, 2012

UJASIRIAMALI WA MAANDAZI - MJINI MOSHI.




Mwana Mama, mkazi wa Mjini Moshi.......akichoma maandazi kwa lengo la kuuza na kujipatia kipato cha kuendesha maisha yake na Familia kwa ujumla. Mama huyu aliyekutwa katika Mtaa wa Riadha Mjini Moshi, ni kielelezo tosha cha namna akina Mama wengi wa Mji wa Moshi wanavyojituma katika kutafuta ridhiki na kuongeza kipato kwa Familia na si kubweteka tu! na kukaa nyumbani pasipo sababu......kusubiri Wanaume wawaletee kila kitu. Mara nyingi wito umekuwa ukitolewa wa kuwataka Wanawake kujishughulisha kwa miradi midogo midogo na mikubwa katika Jamii.

- Picha na Mkuu Mroki a.k.a Father Kidevu.

1 comment:

Anonymous said...

kwakweli kujishughulisha kwa akina mama ni sawa kabisa kuliko kukaa tu umngoje mwanaume alete ni vizuri wote mkajishughulisha kipato kiweze kuongezeka lakini pamoja na huyu mama kujishughulisha ni bora angefanya hii biashara yake katika hali ya usafi maana hapo duh hapo nifumbi tu hiyo hafkeki inaandaliwa katika hali ya uchafu wa hali ya juu sana Mungu analinda walaji huyu mama ameshindwa kufafia hapo na kwagilia maji na wewe awe msafi hata kama anashida usafi hauitaji garama ya aina yoyote hiyo ni uzembe wake tu sahani kaka mwenye glob kama nimekuudhi lakini hii ni kali sana najua huyu mama hasomi hapa maana hana uwezo wa kusoma compyutar sio ya kwamba na mcheka la hasha lakini ingekuwa mimi nimebatika kumwona huyu mama akifanya biasha katika hali hiyo nisingeacha kumwambia ukweli maana mtu ni afya

WATEMBELEAJI