Wednesday, November 2, 2011

LEO NI SIKU YA MAREHEMU WOTE DUNIANI....TUWAOMBEE!

MAKABURI YA CHINI YA ARDHI.

ANGALIA MAKABURI YA WENZETU YA NDANI, KATIKA VIMBA VIMBA!


















Leo ni siku ya marehemu wote duniani, kila ifikapo tarehe 02/11 tunawakumbuka wapendwa wetu wote waliotutangulia mbele ya haki. Kwa namna ya pekee nimepata nafasi ya kutembelea makaburi ya hapa Cesena leo mchana huu, ambapo nimeenda kusali na kuwatembelea marafiki ambao tayari walishatutangulia mbele ya haki. Ili kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu apende kuwaweka miongoni mwa wateule wake mbinguni, na kama bado wanayo mapungufu ya dhambi zao basi waweze kutakaswa, ili hatimaye waonje pendo na huruma ya Mungu.







2 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Wastarehe kwa amani! Amina

Thomas Wambura said...

Baraka. Asante. Nakuona ktk blog yako. Blessed sana

WATEMBELEAJI