Tuesday, February 21, 2012

MTOTO WA WHITNEY HOUSTON...AKUTWA AKIBWIA UNGA.

NEW JERSEY, MAREKANI; Mtoto wa Whitney Houston, Bobbi Kristina Brown.....anadaiwa kufumwa akivuta madawa ya kulevya masaa machache tu baada ya mazishi ya mama yake.

Inadaiwa masaa manne hivi baada ya shughuli za mazishi kumalizika, Bobbi Kristina (18) akiwa na rafiki zake pamoja na ndugu.....ghafla alitoweka na kwenda kusikojulikana. Ingawa mtu wa karibu na familia ya Houston alisema; Kristina....alipelekwa kwenye kituo cha mafunzo ya kuacha dawa za kulevya mwaka jana.
Binti huyu mzuri, amekuwa huku akimuona Mama yake akitumia dawa za kulevya. Familia yake imekuwa na wasiwasi mkubwa wa Kristina kufuata nyayo za Mama yake.

No comments:

WATEMBELEAJI