Tuesday, December 22, 2009

LEO JIONI AMEFARIKI RAFIKI YANGU MPENDWA FERRUCIO.

Mwezi wa saba kabla sijaenda Tanzania: Ferrucio, mimi na mama yake, nyumbani kwao.
Fr.Adolph Majeta kutoka Tz, Ferruccio, baba ya Ferruccio na mimi, nyumbani kwao.

Fr.Adolph, Ferrucio, mama yake na mimi.


Wageni kutoka sehemu nne za Afrika ikiwemo Tanzania, pamoja na Ferruccio na rafiki yake mkubwa Carlo aliye mshika mkono na Guido nyuma. Tulipo kutana pamoja kusherehekea Birthday ya Ferruccio.



FERRUCIO ENZI ZA UHAI WAKE NA RAFIKI YAKE KWENYE BARAFU.
Leo jioni amefariki rafiki yangu mpendwa Ferrucio, ni kijana wa miaka 38 kipofu wa hapa mji ninao kaa Cesena. Ambapo nilikuwa nipatapo tu nafasi nilienda kwao kumtembelea na kumpa kampani na kutembea nae kidogo mjini, maana alihitaji sana kampani, kutokana alihitaji sana msaada wa kukaa pamoja na kuongea. Lakini alipo pata tu ulemavu marafiki wengi vijana walipotea, hawakwenda tena kumtembelea. Mimi nilipo fahamiana nae tu mara nyingi nilikwenda kumtembelea, na sasa nina huzuni maana nilishamzoea sana.
Naamini Mungu atakuwa amempokea kwake.
MUNGU AILAZE ROHO YAKO FERRUCCIO MAHALI PEMA PEPONI, AMINA!




1 comment:

Yasinta Ngonyani said...

Pole sana kwa kufiwa na rafiki yako mpendwa. Mungu ameipokea roho yake na ameilzaza mahali pema peponi. Amina

WATEMBELEAJI