Tuesday, November 16, 2010

WANNE WA FAMILIA MOJA WAFARIKI KATIKA AJALI YA GARI.

Mwishoni mwa wiki iliyopita simanzi na vilio vilitawala kwenye nyumba ya Bwana Francis Mbuya, iliyopo Kimara Baruti, Jijini Dar es salaam...kufuatia ndugu wanne kupoteza maisha yao baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupata ajali, wakati wakitokea Dodoma kurudi Dar es salaam.

Ajali hiyo ilitokea Novemba 7, mwaka huu katika eneo la Masayu Mkoani Morogoro, wakati ndugu hao wakitokea kwenye mahafali ya mmoja kati ya marehemu hao, ambaye ni Berry Lyimo, ambaye alikuwa akisoma Dodoma.
Ajali hiyo ilitokea baada ya gari aina ya Toyota Land Cruiser, lenye namba za usajili T 798 BDG walilokuwa wakisafiria kupasuka tairi la nyuma na kupinduka.

-Mungu azilaze pema peponi roho za marehemu hao... amina!

- Habari Richard Bukos na Issa Mnally.



No comments:

WATEMBELEAJI